Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu

Mfuko wa Fidia kwa Wafanyakazi

WCF Logo
Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
WCF ni Mfuko wenye dhamana ya kulipa fidia kwa wafanyakazi ama wategemezi wao endapo mfanyakazi ataumia, kuugua ama kufariki kutokana na kazi. Aidha, Mfuko una jukumu la kisheria la kukuza mbinu za kuzuia ajali na magonjwa yanayotokana na kazi kwa kushirikiana na OSHA. Aidha, OSHA ni mamlaka yeny...
Ndiyo. Kwa mujibu wa Sheria ya Fidia kwa Wafanyakazi, mwajiri yoyote Tanzania Bara anawajibika kujisajili katika Mfuko.  Mwajiri aliyekuwepo kabla ya tarehe 01 Julai 2015, aliwajibika kujisajili kwenye Mfuko tarehe 01 Julai 2015. Kwa Mwajiri aliyekuwepo baada tarehe 01 Julai 2015, anawajibika k...
Mwajiri anaweza kujisajili katika Mfuko kwa njia ya mtandao (portal.wcf.go.tz) au kwakujaza Fomu za usajili (WCR-1 na WCR-2) na kuziwasilisha kwenye ofisi ya Mfuko iliyopo karibu nae.
Mwajiri anachangia katika Mfuko kwa njia ya mtandao (portal.wcf.go.tz) baada ya kupata kumbukumbu namba ya malipo (control number).
Kwa mujibu wa sheria, Mwajiri ndiye mwenye jukumu la kuchangia kwenye Mfuko. Aidha, ni kosa la jinai kwa mwajiri kumlazimisha mfanyakazi kuchangia kwa namna yoyote kwenye Mfuko.
Mfanyakazi anaweza kumuuliza Mwajiri wake kuhusu kuchangiwa katika Mfuko, pia anaweza kuwasiliana na Mfuko moja kwa moja ili kujua kama mwajiri wake anamchangia.
Mwajiri anachangia asilimia sifuri nukta tano (0.5%) ya mapato ghafi ya wafanyakazi katika sekta ya umma na binafsi
Mapato ghafi ya mfanyakazi yanajumuisha mshahara (basic salary) na posho anazolipwa sambamba na mshahara wa kila mwezi na zisizobadilika.
Viwango vya uchangiaji vipo kwa mujibu wa sheria na vinapatikana baada ya kufanyika kwa Tathmini ya uhimilivu wa Mfuko (Actuarial Valuation).
Michango ya kila mwezi itawasilishwa ndani ya mwezi husika au mwezi unaofuata (kwa mfano michango ya mwezi wa Julai itawasilishwa kabla tarehe 31 Agosti). Aidha, Mwajiri anaweza akalipa kwa miezi mitatu, sita au mwaka lakini baada ya ridhaa ya Mkurugenzi Mkuu wa Mfuko.
Online Help
Adequate And Equitable Compensations
Chati Kupitia Whatapp
Wasiliana nasi kupitia Whatsapp
Unaitaji Msaada
Pata majibu ya hitaji lako hapa
WCF ni Mfuko wenye dhamana ya kulipa fidia kwa wafanyakazi ama wategemezi wao endapo mfanyakazi ataumia, kuugua ama kufariki kutokana na kazi. Aidha, Mfuko una jukumu la kisheria la kukuza mbinu za kuzuia ajali na magonjwa yanayotokana na kazi kwa kushirikiana na OSHA.

Aidha, OSHA ni mamlaka yenye dhamana ya kusimamia usalama na afya mahala pa kazi kwa kuhakikisha waajiri wote nchini wanaweka miundombinu na mifumo inayohakikisha usalama na afya mahala pa kazi vinalindwa.

" >
Ndiyo. Kwa mujibu wa Sheria ya Fidia kwa Wafanyakazi, mwajiri yoyote Tanzania Bara anawajibika kujisajili katika Mfuko.  Mwajiri aliyekuwepo kabla ya tarehe 01 Julai 2015, aliwajibika kujisajili kwenye Mfuko tarehe 01 Julai 2015. Kwa Mwajiri aliyekuwepo baada tarehe 01 Julai 2015, anawajibika kujisajili kwenye mfuko ndani ya siku thelathini (30) baada ya kuajiri mfanyakazi wa kwanza.

" >
Mwajiri anaweza kujisajili katika Mfuko kwa njia ya mtandao (portal.wcf.go.tz) au kwakujaza Fomu za usajili (WCR-1 na WCR-2) na kuziwasilisha kwenye ofisi ya Mfuko iliyopo karibu nae.

" >
Mwajiri anachangia katika Mfuko kwa njia ya mtandao (portal.wcf.go.tz) baada ya kupata kumbukumbu namba ya malipo (control number).

" >
Kwa mujibu wa sheria, Mwajiri ndiye mwenye jukumu la kuchangia kwenye Mfuko. Aidha, ni kosa la jinai kwa mwajiri kumlazimisha mfanyakazi kuchangia kwa namna yoyote kwenye Mfuko.

" >
Mfanyakazi anaweza kumuuliza Mwajiri wake kuhusu kuchangiwa katika Mfuko, pia anaweza kuwasiliana na Mfuko moja kwa moja ili kujua kama mwajiri wake anamchangia.

" >
Mwajiri anachangia asilimia sifuri nukta tano (0.5%) ya mapato ghafi ya wafanyakazi katika sekta ya umma na binafsi

" >
Mapato ghafi ya mfanyakazi yanajumuisha mshahara (basic salary) na posho anazolipwa sambamba na mshahara wa kila mwezi na zisizobadilika.

" >
Viwango vya uchangiaji vipo kwa mujibu wa sheria na vinapatikana baada ya kufanyika kwa Tathmini ya uhimilivu wa Mfuko (Actuarial Valuation).

" >
Michango ya kila mwezi itawasilishwa ndani ya mwezi husika au mwezi unaofuata (kwa mfano michango ya mwezi wa Julai itawasilishwa kabla tarehe 31 Agosti). Aidha, Mwajiri anaweza akalipa kwa miezi mitatu, sita au mwaka lakini baada ya ridhaa ya Mkurugenzi Mkuu wa Mfuko.

" >