Mafao
MAFAO YANAYOTOLEWA NA MFUKO WA FIDIA KWA WAFANYAKAZI
Mfuko wa Fidia kwa Wafanyakazi (WCF) ni Taasisi ya Hifadhi ya Jamii iliyoundwa kwa mujibu wa Kifungu cha 5 cha Sheria ya Fidia kwa Wafanyakazi [Sura 263 marejeo ya mwaka 2015].
Lengo la kuanzishwa kwa Mfuko huu ni kushughulikia masuala ya Fidia kwa Wafanyakazi waliopo katika sekta ya umma na binafsi Tanzania Bara ambao wataumia, kuugua ama kufariki kutokana na kazi wanazozifanya kwa mujibu wa mikataba ya ajira zao.
MAFAO
Mfanyakazi atakapoumia, kuugua ama kufariki kutokana na kazi, Mfuko wa Fidia kwa Wafanyakazi utatoa mafao yafuatayo:
d)Malipo kwa anayemhudumia mgonjwa
e)Huduma za ukarabati na ushauri nasaha
WALENGWA WA MAFAO
Walengwa wa mafao yatakayotolewa na Mfuko ni:
a)Wafanyakazi ambao wataumia au kuugua kutokana na kazi walizoajiriwa nazo
b)Wategemezi wa mfanyakazi atakayefariki kutokana na ajali au ugonjwa uliotokana na kazi