Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu

Mfuko wa Fidia kwa Wafanyakazi

WCF Logo
Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
Mfuko wa Fidia kwa Wafanyakazi (WCF) ni Taasisi ya Hifadhi ya Jamii iliyoundwa kwa mujibu wa Kifungu cha 5 cha Sheria ya Fidia kwa Wafanyakazi [Sura 263]. Lengo la kuanzishwa kwa Mfuko huu ni kushughulikia masuala ya Fidia kwa Wafanyakazi waliopo katika sekta ya umma na binafsi Tanzania Bara ambao w...
Mfuko wa Fidia kwa Wafanyakazi (WCF) ulianza rasmi tarehe 1 Julai 2015 kwa mujibu wa tangazo la Serikali Na.105 la 2011
Malengo ya kuanzishwa kwa Mfuko wa Fidia kwa Wafanyakazi ni pamoja na: Kulipa fidia himilivu na stahiki kwa wafanyakazi watakaoumia ama kuugua kutokana na kazi walizoajiriwa nazo au kulipa fidia kwa wategemezi endapo Mfanyakazi atafariki kutokana na ajali ama ugonjwa uliosababishwa na kazi ali...
Majukumu ya Mfuko wa Fidia kwa Wafanyakazi ni pamoja na: Kusajili waajiri Kufanya tathmini ya mazingira hatarishi mahala pa kazi Kukusanya na kupokea michango kutoka kwa waajiri Kuwekeza michango itakayokusanywa Kulipa fidia stahiki Kutunza kumbukumbu za matukio ya ajali, magonjwa na...
Ni waajiri na wafanyakazi wote katika Sekta ya Umma na Binafsi Tanzania Bara.
Wajibu na Majukumu ya Mwajiri katika Mfuko ni kama yafuatayo: Kujisajili katika Mfuko; Kulipa michango katika Mfuko kwa wakati; Kuwasilisha taarifa za mapato ya mwaka ya wafanyakazi; Kuhakikisha wakandarasi wanaowatumia wanazingatia Sheria ya Fidia kwa Wafanyakazi wakati wa utekelezaji...
Wajibu wa Mfanyakazi katika Mfuko ni: Kutoa taarifa kwa wakati kwa mwajiri au Mkurugenzi Mkuu pindi atakapopatwa na ajali au kubainika kuwa na ugonjwa unaotokana na kazi; Kutoa ushirikiano pindi atakapohitajika kufanyiwa uchunguzi wa kitabibu; Kuzingatia maelekezo yanayotolewa na Mamlaka...
Mwajiri ana wajibu wa kuweka cheti cha usajili sehemu ambayo wafanyakazi wanaweza kukiona kwa urahisi kwa lengo kujua kuwa mwajiri wao amejisajili. Aidha, mfanyakazi ana haki ya kuwasiliana na Mfuko moja kwa moja ili kupata uhakika endapo mwajiri wake amejisajili.
Mwajiri ananufaika na Mfuko kama ifuatavyo; Kuwa na uhakika wa kinga ya wafanyakazi wake dhidi ya majanga (ajali, ugonjwa au kifo) yanayoweza kuwapata kutokana na kazi ili kuongezeka kwa tija katika uzalishaji; Kupungua kwa gharama za ufuatiliaji wa madai ya fidia zilizokuwepo mwanzo kabla...
Tofauti baina ya WCF na mifuko mingine ni; 1. Madhumuni; WCF ni Mfuko wenye dhamana ya kulipa fidia kwa wafanyakazi ama wategemezi wao endapo mfanyakazi ataumia, kuugua ama kufariki kutokana na kazi. Aidha, Mifuko ya Pensheni, mathalani NSSF au PSSSF, ina dhamana ya kulipa mafao ya uzeeni p...
Online Help
Adequate And Equitable Compensations
Chati Kupitia Whatapp
Wasiliana nasi kupitia Whatsapp
Unaitaji Msaada
Pata majibu ya hitaji lako hapa
Mfuko wa Fidia kwa Wafanyakazi (WCF) ni Taasisi ya Hifadhi ya Jamii iliyoundwa kwa mujibu wa Kifungu cha 5 cha Sheria ya Fidia kwa Wafanyakazi [Sura 263]. Lengo la kuanzishwa kwa Mfuko huu ni kushughulikia masuala ya Fidia kwa Wafanyakazi waliopo katika sekta ya umma na binafsi Tanzania Bara ambao wataumia, kuugua ama kufariki kutokana na kazi wanazozifanya kwa mujibu wa mikataba ya ajira zao.

" >
Mfuko wa Fidia kwa Wafanyakazi (WCF) ulianza rasmi tarehe 1 Julai 2015 kwa mujibu wa tangazo la Serikali Na.105 la 2011

" >
Malengo ya kuanzishwa kwa Mfuko wa Fidia kwa Wafanyakazi ni pamoja na:

  1. Kulipa fidia himilivu na stahiki kwa wafanyakazi watakaoumia ama kuugua kutokana na kazi walizoajiriwa nazo au kulipa fidia kwa wategemezi endapo Mfanyakazi atafariki kutokana na ajali ama ugonjwa uliosababishwa na kazi aliyoajiriwa nayo;
  2. Kutekeleza matakwa ya Sera ya Hifadhi ya Jamii ya mwaka 2003;
  3. Kutoa huduma ya utengemao;
  4. Kuweka utaratibu utakaowezesha kuharakisha malipo ya fidia kwa wafanyakazi na wategemezi wao;
  5. Kuweka utaratibu mzuri wa kupokea michango kutoka kwa waajiri na kufanya malipo;
  6. Kukidhi matakwa ya Mikataba ya Kimataifa inayohusu fidia kwa wafanyakazi; 
  7. Kukuza mbinu za kupambana na kuzuia ajali, magonjwa na vifo mahala pa kazi.
" >
Majukumu ya Mfuko wa Fidia kwa Wafanyakazi ni pamoja na:

  1. Kusajili waajiri
  2. Kufanya tathmini ya mazingira hatarishi mahala pa kazi
  3. Kukusanya na kupokea michango kutoka kwa waajiri
  4. Kuwekeza michango itakayokusanywa
  5. Kulipa fidia stahiki
  6. Kutunza kumbukumbu za matukio ya ajali, magonjwa na vifo mahala pa kazi
  7. Kukuza mbinu za kuzuia ajali, magonjwa ama vifo kutokana na kazi
  8. Kutoa elimu kwa Umma kuhusu Mfuko
" >
Ni waajiri na wafanyakazi wote katika Sekta ya Umma na Binafsi Tanzania Bara.

" >
Wajibu na Majukumu ya Mwajiri katika Mfuko ni kama yafuatayo:

  1. Kujisajili katika Mfuko;
  2. Kulipa michango katika Mfuko kwa wakati;
  3. Kuwasilisha taarifa za mapato ya mwaka ya wafanyakazi;
  4. Kuhakikisha wakandarasi wanaowatumia wanazingatia Sheria ya Fidia kwa Wafanyakazi wakati wa utekelezaji wa majukumu ya kimkataba baina yao;
  5. Kuimarisha usalama na afya mahala pa kazi;
  6. Kutoa taarifa pindi mfanyakazi anapoumia, anapougua au kufariki kutokana na kazi;
  7. Kutunza kumbukumbu na kuwasilisha taarifa za matukio ya ajali, magonjwa yanayotokana na kazi au vifo katika Mfuko kwa wakati;
  8. Kuwasilisha katika Mfuko madai ya fidia kwa wafanyakazi kwa wakati pamoja na vielelezo vinavyohusu madai hayo;
  9. Kuwafahamisha wafanyakazi kuhusu haki zinazohusiana na masuala ya fidia kwa wafanyakazi kwa kuweka tamko linalohusu haki za wafanyakazi katika maeneo yao ya kazi na sehemu ambayo inaweza kusomeka;
  10. Kuweka sehemu wazi cheti cha usajili katika Mfuko ili wafanyakazi wajue kuwa mwajiri wao amejisajili;
  11. Kutoa taarifa yoyote katika Mfuko inayo muhusu Mfanyakazi au mtegemezi wa Mfanyakazi inayoweza kuathiri ulipaji wa fidia;
  12. Kutoa taarifa katika Mfuko kuhusu mabadiliko yoyote ya taarifa za mwajiri au wafanyakazi;
  13. Kutoa ushirikiano kwa Mfuko katika utekelezaji wa Sheria ya Fidia kwa Wafanyakazi.
" >
Wajibu wa Mfanyakazi katika Mfuko ni:

  1. Kutoa taarifa kwa wakati kwa mwajiri au Mkurugenzi Mkuu pindi atakapopatwa na ajali au kubainika kuwa na ugonjwa unaotokana na kazi;
  2. Kutoa ushirikiano pindi atakapohitajika kufanyiwa uchunguzi wa kitabibu;
  3. Kuzingatia maelekezo yanayotolewa na Mamlaka mbalimbali kuhusu usalama mahali pa kazi
  4. Kuzingatia Sheria, Kanuni, Taratibu na Miongozo mbalimbali kuhusu masuala ya fidia kwa wafanyakazi;
  5. Kutunza kumbukumbu binafsi zinazohusu masuala ya kazi;
  6. Kutoa ushirikiano kwa Mfuko katika utekelezaji wa Sheria ya Fidia kwa Wafanyakazi.
" >
Mwajiri ana wajibu wa kuweka cheti cha usajili sehemu ambayo wafanyakazi wanaweza kukiona kwa urahisi kwa lengo kujua kuwa mwajiri wao amejisajili. Aidha, mfanyakazi ana haki ya kuwasiliana na Mfuko moja kwa moja ili kupata uhakika endapo mwajiri wake amejisajili.

" >
Mwajiri ananufaika na Mfuko kama ifuatavyo;

  1. Kuwa na uhakika wa kinga ya wafanyakazi wake dhidi ya majanga (ajali, ugonjwa au kifo) yanayoweza kuwapata kutokana na kazi ili kuongezeka kwa tija katika uzalishaji;
  2. Kupungua kwa gharama za ufuatiliaji wa madai ya fidia zilizokuwepo mwanzo kabla ya kuanza kwa Mfuko;
  3. Kupata ushauri wa kitaalamu kuhusiana na usalama mahali pa kazi;
" >
Tofauti baina ya WCF na mifuko mingine ni;

1. Madhumuni;

WCF ni Mfuko wenye dhamana ya kulipa fidia kwa wafanyakazi ama wategemezi wao endapo mfanyakazi ataumia, kuugua ama kufariki kutokana na kazi.

Aidha, Mifuko ya Pensheni, mathalani NSSF au PSSSF, ina dhamana ya kulipa mafao ya uzeeni pindi mfanyakazi anapostaafu kwa hiari au lazima.

Kwa upande mwingine, Mfuko wa Bima ya Afya mathalani NHIF una dhamana ya kutoa Bima ya matibabu kwa magonjwa yasiyotokana na kazi.

2. Uchangiaji;

Katika Mfuko wa WCF jukumu la uchangiaji ni la mwajiri pekee, wakati katika Mifuko mingine (PSSSF, NSSF & NHIF) jukumu la kuchangia lipo kwa Mwajiri na Mfanyakazi.

" >