Kuanzishwa
UTANGULIZI
Mfuko wa Fidia kwa Wafanyakazi (WCF) ni Taasisi ya Hifadhi ya Jamii iliyoundwa kwa mujibu wa Kifungu cha 5 cha Sheria ya Fidia kwa Wafanyakazi [Sura 263 marejeo ya mwaka 2015] na inahusu waajiri na waajiriwa wote Tanzania Bara..
Lengo la kuanzishwa kwa Mfuko huu ni kushughulikia masuala ya Fidia kwa Wafanyakazi waliopo katika sekta ya umma na binafsi ambao wataumia, kuugua ama kufariki kutokana na kazi wanazozifanya kwa mujibu wa mikataba ya ajira zao.
DIRA
Mfano wa kuigwa katika utoaji wa huduma za fidia kwa wafanyakazi barani Afrika.
DHIMA
Kupunguza athari za kijamii na kiuchumi za majanga yatokanayo na kazi kwa wafanyakazi, familia zao na waajiri kwa kutoa fidia stahiki, kwa usawa, uendelevu na ufanisi.
MAADILI
a)Uadilifu
b)Ushirikiano katika kazi
c)Uwajibikaji
d)Ufanisi
e)Kuwajali wanachama
MALENGO
Malengo ya kuanzishwa kwa Mfuko wa Fidia kwa Wafanyakazi ni pamoja na:
a)Kulipa fidia himilivu na stahiki kwa wafanyakazi watakaoumia ama kuugua kutokana na kazi walizoajiriwa nazo au kulipa fidia kwa wategemezi endapo Mfanyakazi atafariki kutokana na ajali ama ugonjwa uliosababishwa na kazi aliyoajiriwa nayo;
b)Kutekeleza matakwa ya Sera ya Hifadhi ya Jamii ya mwaka 2003;
c)Kutekeleza matakwa ya kifungu cha 5 cha Sheria ya Fidia kwa Wafanyakazi [Sura 263 Marejeo ya Mwaka 2015];
d)Kutoa huduma ya utengemao;
e)Kuweka utaratibu utakaowezesha kuharakisha malipo ya fidia kwa wafanyakazi na wategemezi wao;
f)Kuweka utaratibu mzuri wa kupokea michango kutoka kwa waajiri na kufanya malipo;
g)Kukidhi matakwa ya Mikataba ya Kimataifa inayohusu fidia kwa wafanyakazi;
h)Kukuza mbinu za kupambana na kuzuia ajali, magonjwa na vifo mahala pa kazi.
MAJUKUMU
Majukumu ya Mfuko wa Fidia kwa Wafanyakazi ni kama yafuatayo:
a)Kusajili waajiri Tanzania Bara;
b)Kufanya tathmini ya mazingira hatarishi mahala pa kazi;
c)Kukusanya na kupokea michango kutoka kwa waajiri;
d)Kuwekeza fedha zilizopo;
e)Kulipa fidia;
f)Kutunza kumbukumbu za matukio ya ajali, magonjwa na vifo mahala pa kazi;
g)Kukuza mbinu za kuzuia ajali, magonjwa ama vifo vinavyotokana na kazi;
h)Kutoa elimu kwa Umma;